JP Magufuli: Nataka niwe kama Mzee Kikwete
Magufuli ameomba apewe tena miaka mitano ili aonyeshe dunia itakavyokwenda.
“Amekuja Mzee Kikwete mmepima kwa miaka 10, mimi miaka mitano ndio maana nawaomba mnipe tena miaka mitano, tuone dunia itakavyokwenda,” amesema Dk. Magufuli.
Amesema, katika kipindi cha miaka mitano ya uongozi wake, ameleta maendeleo licha ya kwamba baadhi ya watu wanabeza utendaji wake.
Tunaingia awamu ya pili ya uchumi, hakuna alietegemea pale Maswa kuwe na viwanda vya chaki, hapa Muwena barabara ya lami nzuri na wanapita watu wa vyama vyote.
“Hata wanaotukana wanapita hapa hapa, shukrani ya punda ni mateke lakini sisi wajibu wetu nikufanya kazi kwa ajili ya Watanzania wote,” amesema Rais Magufuli.
Dk. Magufuli amewaomba wana CCM na Watanzania kwa ujumla kumchagua kwa kuwa, maendeleo hayana chama.
“Ndio maana nawaomba wana CCM wenzangu na wa vyama vingine mtupe kura, sababu maendeleo hayana chama,” amesema.


Comments
Post a Comment